Kwa kuzingatia
Kanuni za Uchaguzi za Baraza la Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ,
Tangazo la Serikali Na. 95/2016, Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Mashirika
Yasiyo ya Kiserikali inapenda kuyajulisha Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuwa
kutakuwa na uchaguzi wa viongozi na wajumbe wa Baraza kutokana na Baraza la
sasa kumaliza muda wake. Kwa tangazo hili wadau wa Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali yaliyosajiliwa wanatakiwa kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi huu
utakaofanyika kama ifuatavyo:
1.
Ngazi ya Wilaya tarehe 11 Agosti, 2016.
2.
Ngazi
ya Mkoa tarehe 17 Agosti, 2016.
3.
Ngazi
ya Taifa tarehe 23 Agosti, 2016.
Maelekezo mengine kuhusu uchaguzi tajwa
yatatolewa na wasimamizi wa uchaguzi wa ngazi husika.
Imetolewa kwa niaba ya Kamati Tendaji leo 8
Mwezi Julai, 2016.
Ismail A. Suleiman
KATIBU
MKUU
BARAZA
LA TAIFA LA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (NaCoNGO)
0 comments:
Post a Comment