Saturday, 30 April 2016

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto, S. Nkinga akiwa na wajumbe wa Baraza la Watoto Jamhuri ya Muungano wa Tanzania muda mfupi baada ya ufunguzi wa mkutano wa Baraza. Watatu kutoka kulia ni mwenyekiti wa Baraza, Ameir Haji Khamis pamoja na wajumbe wengine.Mkutano huo unafanyika katika ukumbi wa Msimbazi Center, Jijini Dar es salaam, kuanzia tarehe 27- 29,Aprili, 2016

Katika kikao cha Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuliweza kukutana na mtoto Getrude Clemency mkazi wa mkoani Mwanza, ambaye hivi karibuni aliwakilisha Tanzania kwenye Mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa lililofanyika New York Marekani. Wakati akihojiwa na BBC Getrude aliweza kuongea maneno yafuatayo kuhusu uwakilishi wake, shughuli anazofanya na Agenda aliyowasilisha katika Baraza la Umoja wa Mataifa. endelea …
Katika kikundi chetu tunashughulikia na kujadili, Haki za Watoto na Agenda ya Mtoto na masuala mbalimbali yanayowaguza watoto, tunakuwa na mada na kuijadili kwa siku hiyo. Lakini vile vile kuelezea matukio mbalimbali ambayo yametukia kwa watoto kwa muda wa wiki nzima.
Katika shughuli zetu za mtandao wa wanahabari watoto, kwa kushirikiana na program ya kazi tumeweza kutembelea maeneo mbalimbali ambayo yameweza kuathirika na mabadiiko ya tabia ya nchi lakini na vile vile uchafuzi wa mazingira.
Katika maeneo yale  tumekuwa tunatembea na tunapiga picha maeneo, tukisha piga picha tunawauliza wale watu wanaolizunguka lile eneo na viongozi wao, tukimaliza tunaenda katika mitandao ya kijamii, kuna ramani, ambapo watu wote duniani wanaweza kusoma kinachoendelea Tanzania na kuangalia.
Lakini vile vile kipindi hicho hicho tunachoenda kupiga picha maeneo hayo, hicho kipindi tunakitumia katika kurusha katika vipindi vyetu mbalimbali vya redio na TV ambavyo tunavifanya mjini Mwanza na kuelimisha watu zaidi kuhusiana na mabailiko ya tabia ya nchi na athari zake katika jamii inayozunguka.
Progamu hizo tunazozifanya, ndizo zilizonifanya nikachaguliwa kwenda kuwakilisha vijana na watoto Dunia nzima kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi, na kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusiana na vijana wananguvu ya kusimama na kuelezea kuhusiana na mambo ambayo yanawakumba, kuhusiana na mabadiliko ya tabia ya nchi, na pia wanao uwezo wa kusimama na kuchukua hatua kuhusiana na vitu vinavyowakabili, hususan kuhusiana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Niliweza kueleza viongozi kuwa wanatakiwa wakisha saini mkataba wa kazi kitu kinachofuata ni kuchukua hatua siyo kusubiri mpaka matokeo makubwa kabisa yametokea ndio wanachukua hatua. Wanatakiwa kuchukua hatua kuanzia sasa hivi ili kuweza kutokomeza kabisa athari za tabia ya nchi kama tunavyozifahamu.
Athari kubwa kabisa zinawakumba watoto zaidi katika jamii. Ukisikia ukame na mafuriko katika vyombo vya habari watoto ndio wanaoathirika zaidi. Ndio maana niliweza kuwashawishi wale viongozi kuwa wakisha saini ule mkataba wasisubiri muda mrefu kutekeleza, wachukue hatua pale pale njia madhubuti za kupanaga kuepukana na mabadiliko ya tabia ya nchi katika jamii.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto, S. Nkinga akiwa na wajumbe wa Baraza la Watoto Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mtoto Getrude Clemency (wa pili kushoto- mstari wa mbele) mkazi wa mkoani Mwanza ambaye hivi karibuni aliwakilisha Tanzania kwenye Mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa lililofanyika New York Marekani kuzungumzia athari za tabia nchi. Wengine ni wajumbe wa Baraza la Watoto Tanzania Bara na Zanzibar, wanohudhuria mkutano wa Baraza la Watoto katika ukumbi wa Msimbazi Center, Jijini Dar es salaam, kuanzia tarehe 27- 29,Aprili, 2016

0 comments:

Post a Comment