Tuesday, 2 February 2016

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
(TAARIFA KWA UMMA)
Taarifa inatolewa kwa umma kwamba Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao chake cha 38 kilichofanyika tarehe 27 Januari, 2016 iliazimia kufuta usajili wa Shirika la Kuleana Centre for Children’s Rights kutokana na kukiuka masharti ya Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005). Kwa tangazo la taarifa hii, shughuli za Shirika tajwa zimekoma kuanzia tarehe ya taarifa hii. Wanachama wa shirika wanaagizwa kufunga shughuli za shirika na kuzingatia taratibu za ufungaji wa shughuli za Shirika kama zinavyoainishwa katika katiba ya Shirika na Kanuni za Sheria ya NGOs, GN.Na.8 ya Mwaka 2015.

M.S.Katemba
MSAJILI WA NGOs
2 Februari, 2016



0 comments:

Post a Comment